Pages

Friday, July 12, 2013

Habari za Kimataifa

HUYU NDIYE RAIS MWENYE KIPATO KIDOGO KULIKO WOTE DUNIANI

Mjue raisi mwenye kipato kidogo zaidi Duniani


Jose Alberto Mujica maarufu kama PEPE, Kama wewe ni mfuatiliaji wa siasa na habari za kimataifa basi huwezi kukosa kusikia jina ili likitajwa popote pale…..
Jose Rais wa Uruguay aliezaliwa tarehe ya 20 mwezi wa tano mwaka 1930. Rais huyo wa Uruguay ndie Rais mwenye kipato kidogo kuliko wote duniani…!!
Hii inatokana na asilimia 90 ya mapato yake Mujica kuamua kutoa msaada kwa wananchi wa nchi yake wasiojiweza
kwa asilimia 10….
Mujica ambae ni mtoto wa mkulima alitawala Uruguay mnamo mwaka 2009, lakini kabla ya hapo ni mwanaharakati wa kimapinduzi ndani ya mwaka wa 1969 yeye na chama chake walipoamua kupigania haki na sheria ya uruguay… Mwaka 1974 alifungwa baada ya kuanzishwa kwa chama ambacho kwa muda mchache kilikuwa kinasumbua sana kiasi kwamba kuleta mtafaruku wa kutawaliwa na wazungu alienda jela na kupewa adhabu ya kupasua kokote kwa kipindi chote akiwemo jela…. Mwaka 1985 aliachwa Uhuru baada ya hapo aliendeleza falsafa yake hadi mwaka 2009 alipoamua kugombea urais na kufanikiwa kushinda kiti hicho na kuiongoza Uruguay…!! Mujica anatazamiwa kwa mujibu wa Jarida la Forbes ndie Rais mwenye kipato kidogo zaidi dunia kupitia marais wote waliopo kwenye umoja wa Mataifa…!!

Rais Hugo Chavez enzi za uhai wake na Rais Mujica wakisalimiana…

No comments:

Post a Comment