Pages

Thursday, July 18, 2013

Maurinho asisitiza


Tunayemtaka ni Wayne Rooney tuu..!! - Mourinho


Jose Mourinho akiteta jambo na mkurugenzi wa Chelsea Ron Gourlay huko Bangkok , Thailand . 
 
Kocha wa Chelsea Jose Morinho amethibitisha dhamira ya kumsajili 
mshambuliaji wa Manchester United Wayne Rooney 
baada ya kutoa kauli kuwa ” 
Tunayemtaka ni Wayne Rooney pekee”. 
Kauli hii inakuja huku zikiwa zimepita saa chache baada ya Manchester United 
kuikataa ofa ya Chelsea ya Paundi milioni 10 kwa ajli ya mchezaji huyo . 
Jose Mourinho akiteta jambo na mkurugenzi wa Chelsea Ron Gourlay huko Bangkok , Thailand .
Hata hivyo Chelsea imezikanusha taarifa kuwa Ilikuwa Tayari kuwatoa mmojawapo kati ya David Luiz na Juan Matta kama sehemu ya dili la kumnunua Rooney. Mustakabali wa Rooney unaonekana kuwa story ya “Msimu huu wa usajili” baada ya kuwepo na kauli tata juu ya maisha ya mchezaji huyo ndani ya klabu ya ya Manchester United .
Pamoja na haya , bado mabingwa hawa wa England (United) wameendelea kushikilia msimamo wao kuwa mchezaji huyo hauzwi .

No comments:

Post a Comment