Pages

Friday, July 12, 2013

Kutoka Anfield

LIVERPOOL YAMUWEKEA NGUMU LUIS SUAREZ BILA PAUNI MILIONI 40 HAONDOKI

LIVERPOOL haitakubali ofa yoyote chini ya pauni milioni 40 kwa ajili ya kumuuza mshambuliaji wake raia wa Uruguay, Luis Suarez anayetaka kuondoka Anfield.

Jumatano iliyopita iliripotiwa kuwa miamba ya Hispania, Real Madrid inajipanga kupeleka ofa ya pauni milioni 40 baada ya ofa ya Arsenal ya pauni milioni 30 kutolewa nje.

Arsenal ambayo imeamua kumfanya Suarez lengo lake kuu la usajili baada ya kuonekana kukwama kumtwaa mshambuliaji wa Madrid, Gonzalo Higuain ambaye kocha wake mpya Carlo Ancelotti anataka kumbakisha, inaelezwa kujipanga kupeleka ofa nyingine ya pauni milioni 35.

Lakini bado Arsene Wenger anakabiliwa na kizingiti kwa kuwa Liverpool haitakubali ofa ya chini ya pauni milioni 40, na kwa kuwa mkataba wa Suarez unakwenda hadi mwaka 2016, klabu hiyo haina presha ya kumuuza – licha ya matakwa yake.

Suarez, 26, atakosa mechi sita za kwanza za msimu mpya wa Premier League wakati akimaliza adhabu ya kukosa mechi kumi msimu uliopita baada ya kumng’ata beki wa Chelsea, Branislav Ivanovic na anatarajiwa kujiunga na kikosi chake wiki ijayo

No comments:

Post a Comment