Pages

Thursday, July 18, 2013

Unayafahamu haya.....


Pokea Haya Maujanja 15

Number 15

1. Wafungwa walioko kwenye gereza la watu wenye makosa ya ugaidi huko Guantanamo bay cuba hupewa misosi ya nguvu toka kwenye migahawa ya McDonalds pale wanapoonyesha ushirikiano wa kufichua siri wakati wakihojiwa.

2.Unaweza kutibu maumivu ya kichwa kwa kusugua kipisi cha limao kwenye paji la uso.

3. Inasemekana kuwa asilimia 60 ya wanawake walioko ndani ya ndoa afya yao kimwili na kiakili sio nzuri kutokana na matatizo yanayohusiana na ndoa.

4.Hii inawahusu wale watu ambao wanapenda sana kuchat kwenye simu zao mpaka kufikia kusikia milio ya simu au vibration vichwani mwao hata pale ambapo hakuna msg au simu iliyopigwa, watu hawa wanaugua ugonjwa wa kisaikolojia unaitwa TEXTAPHRENIA.

5. Producer Dr. Dre hakuwahi kufahamu au kugundua kama Eminem ni mzungu mpaka siku waliyokutana.

6. Wanawake ambao hukumbwa na msongo wa mawazo wakati wa uja uzito wao wana hatihati ya kuzaa watoto wenye hasira kali.

7. Unaambiwa kwa kila hatua moja ambayo unatembea unatumia misuli 200 ambayo yote kwa pamoja hukusaidia kuitengeneza hiyo hatua.

8. Wakati Mohamed Ali anaanza kuingia kwenye mchezo wa ngumi, Mwalimu wake ambaye alikuwa mzungu alimkatisha tamaa akimwambia kuwa hawezi kufanikiwa kwenye mchezo huo… hiki kitendo kilimpa hasira bondia huyu na alipofanikiwa kushinda medali yake ya kwanza ya OLYMPIC alimzawadia mwalimu huyu na kumkumbusha maneno yake, hii ni fundisho kwa kila mmoja kwamba usikubali mtu akukatishe tamaa kwenye ndoto yako.

9. Marapa wawili toka New York Busta Rhymez na Jay Z waliowahi pia kuja Tanzania kufanya matamasha kwa hisani ya Clouds Fm na Prime time promotions, waliwahi kusoma shule moja ya sekondari na siku moja walishindansishwa kwenye zile rap freestyles kwenye Mgahawa wa shule hiyo na Jay Z aliibuka mshindi, kitambo sana ilikuwa… rapa mwingine ambae ni Christopher Wallace au Notorious BIG naye alikuwa mwanafunzi kwenye hiyo shule.

10. Hii ni kwa watu wangu wanaovuta fegi au sigara, Unaambiwa kila sigara moja unayovuta inapunguza urefu wa maisha yako kwa angalau dakika kumi na moja .

11. Mitandao ya ngono imekuwa moja ya biashara zinazoongoza kwa kuingiza fedha kutumia Internet ambapo katika kila sekunde kuna dola elfu tatu na sabini na tano za kimarekani hutumiwa kwenye mitandao hiyo.

12. Unaambiwa Jina maarufu la kiume kuliko majina yote ulimwenguni ni Mohamed, inakadiriwa kuwa kuna Wanaume zaidi ya milioni 150 duniani waliopewa hili jina.. Muhammad was the most common baby boy name in England and Wales in 2009, 2011 and 2012 and the second most popular in 2007 and 2010, combining 14 spelling variations

13. Mvumbuzi wa balbu au taa Tomas Edison Alva alikuwa muoga sana wa giza na ndio maana akafanya juu chini mpaka akatengeneza taa.

14. Mwanadamu huzaliwa na mifupa 300 mwilini mwake lakini mpaka anafikia hatua ya utu uzima hubakiwa na mifupa 206 pekee, unaambiwa hiyo mingine inapungua kutokana na kuunganika kadri umri unavyosogea.

15. Enzi za kale nchini Uingereza kulikuwa na sheria inayoitwa sheria ya dole gumba au The rule of the thumb ambayo ilikuwa inaamuru kuwa mwanaume au mume kutoruhusiwa kumpiga mkewe na kitu kikubwa zaidi ya kidole gumba.

No comments:

Post a Comment