Pages

Thursday, July 18, 2013

Huyu ndiye....

 Mmarekani wa kwanza kuwahi kumiliki Mabilioni ya Dola

us_20_21_pic_ rockefeller_john_d_1884
John Davison Rockefeller aliwahi kushikilia rekodi ya kuwa Mwanaume tajiri duniani lakini pia Muamerika wa kwanza kuwahi kumiliki mabilioni ya dola ambapo mwaka 2007 mtandao wa Forbes ulirekebisha utajiri wa John Rockefeller baada ya mfumuko wa bei na kukadiria kwamba alikuwa na utajiri wa dolla billion 663.4
Unaambiwa In 1870, he founded Standard Oil Company and aggressively ran it until he officially retired in 1897
John Rockefeller alifariki mwaka 1937 May 23 huko Florida akiwa na miaka 97, utajiri wake umetokana sana na biashara ya mafuta ambayo kwa kipindi hicho ndiyo ilikuwa nishati mpya na inahitajika sana, alianzisha kampuni inaitwa Standard Oil Company ambayo iliweza kufanikiwa kutawala soko la mafuta kwa kiasi kikubwa sana, baada ya biashara kwenda vizuri akiwa na ndugu zake wa karibu… John Rockefeller aliweza kuwa Mmarekani wa kwanza kufikisha utajiri wa dola billioni moja.
Zaidi ya biashara, John Rockerfeller alitumia utajiri wake mwingi kwenye ku-invest ndani ya masuala ya utafiti wa kisayansi kwenye mambo ya dawa za binadamu, elimu na kusaidia watu kwenye foundation yake ambapo kwenye research alizowahi kuwekeza pesa zake na kuweza kupata mafanikio makubwa hasa kwenye kutokomeza janga la homa ya manjano kipindi hicho na minyoo inayoitwa hookworm.
Kumbukumbu ya John Rockefeller kwenye sekta ya elimu bado ipo hadi leo kwasababu ndiye mwazilishi wa vyuo vikuu Marekani kama University of Chicago na Rockerfeller University.

No comments:

Post a Comment