Pages

Friday, July 12, 2013

Kutoka Cairo

WAFUASI WA MORSI WAANDAMANA CAIRO


Wafuasi wa rais wa zamani wa Misri Mohamed Morsi
Wafuasi wa rais wa Misri aliyeondolewa madarakani Mohammed Morsi wamefanya maandamano makubwa mjini Cairo, huku waumini wa dini ya Kiislamu wakiadhimsiha Ijumaa ya kwanza tangu kuanza kwa mwezi mtukufu wa Ramadhan.
Wafuasi wa kiongozi huyo wa vugu vugu la Muslim Brotherhood walijikusanya Mashariki mwa mji huo, kushinikiza utawala wa kijeshi kumrejesha madarakani kiongozi wao.
Wapinzani wa rais huyo wa zamani ambao waliandamana hadi rais huyo akaondolewa madarakani na jeshi watakusanyika katika medani ya Tahrir.
Watu kadhaa wameuawa kwenye ghasia zilizotokea tangu Morsi alipoondolewa.
Mwandishi wa BBC mjini Cairo, Jim Muir anasema vuguvugu la Muslim Brotherhood huenda liliwatenga raia wengi wakati wa utawala wa Morsi, lakini bado raia wengi wa nchi hiyo hawataki jeshi kuingilia masuala ya siasa.

Marekani kutuma ndege za kivita Misri

Siku ya Alhamisi serikali ya Marekani, ilitoa wito kwa utawala mpya wa Misri, kusitisha harakati zake za kuwakamata wanachama wa vuguvugu la Muslim Brotherhood na kuonya dhidi ya kulenga kundi lolote.
Wanajeshi wakishika doria mjini Cairo
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon vile vile ameonya utawala huo wa Misri kutotenga chama chochote cha kisiasa katika harakati za kutatua mzozo wa kisiasa unaokumba taifa hilo.

No comments:

Post a Comment