Obama kutembelea Africa
White  House imesema kuwa rais wa Marekani Barack Obama atakwenda Afrika  mwishoni mwa mwezi wa sita ambapo atazuru nchi tatu.
Katika taarifa Jumatatu jioni, White House  ilisema rais Obama na mke
 wake Michelle watakwenda Senegal,  Afrika Kusini na Tanzania mwishoni 
mwa Juni na mapema mwezi Julai.
Utawala wa rais Obama  unasema rais huyu wa Marekani atakutana na 
maafisa wa serikali, viongozi wa kibiashara, asasi za kiraia na makundi 
ya vijana.
Safari ya bw.Obama itaanza Juni 26 mpaka Julai 3 na inalenga 
kudhihirisha mahusiano ya karibu kati ya Marekani na nchi za Afrika, 
kusini mwa jangwa la Sahara.
Rais Obama ambaye baba yake alizaliwa Kenya, alizuru Afrika  mara 
moja  katika muhula wake wa kwanza, alipotembelelea Ghana mwaka 2009.
Mkewe Michelle Obama pia amesafiri kwenda Afrika Kusini na Bostwana.
  

No comments:
Post a Comment