BAN KI-MOON ALAANI SHERIA YA HABARI YA BURUNDI

Katibu
 Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon ameikosoa sheria mpya 
iliyopitishwa na serikali ya Burundi, ambayo amesema itaathiri uhuru wa 
vyombo vya habari.
Rais 
Pierre Nkurunziza, siku ya Jumanne aliridhia sheria hiyo, ambayo 
imekosolewa vikali na mashirika ya habari na yale ya haki za binaadamu.
Msemaji
 wa Umoja wa Mataifa Martin Nesirky, alisema Katibu Mkuu Ban 
amesikitishwa na sheria hiyo, yenye vifungu vinavyoweza kukandamiza 
uhuru wa habari, huku akisisitiza kuwa haki ya uhuru ya kujieleza na 
sekta huru ya habari ni mambo muhimu kwa ustawi wa demokrasia.
Sheria
 hiyo iliyopitishwa na bunge la Burundi mwezi April, inadhoofisha ulinzi
 wa vyanzo vya habari, inadhibiti kuripoti habari za uchunguzi, na 
inawataka waandishi wote kuwa na shahada ya Chuo Kikuu bila kujali 
uzoefu.
Pia 
inapiga marufuku kusambaza taarifa au nyaraka kuhusu mada za ulinzi au 
taarifa zinazochukuliwa kuwa propaganda za adui, au zinazoweza kuathiri 
uchumi wa Burundi.
Shirka
 la kutetea haki za waandishi la Reporters Without Boarders limeielezea 
sheria hiyo kuwa ni alama ya siku nyeusi kwa uhuru wa habari nchini 
Burundi.
No comments:
Post a Comment