1. Kwanza husukuma ndani zaidi uchafu 
 sikioni(ear wax),ule utando unaotoka ndani
 ya sikio.
 Unapochokonoa sikio kwa pamba huupeleka
 uchafu kuingia ndani zaidi ya sikio, hii
 husababisha vijidudu kushambulia kuta za
 ndani ya sikio na ngoma ya sikio, hupelekea
 mtu kutosikia vizuri.
 2. Pia kutumia pamba kusafishia sikio
 huatarisha kutokwa damu masikioni.
 Unaposukuma ndani zaidi pamba kwenye
 kuta za sikio ni ngozi laini, unaweza kuona
 viti damu kwenye pamba, hii hutokana na
 pamba kukwangua kuta za sikio lako.
 3. Kutoka maji maji yanayowasha au usaha
 sikio.
 Hizi pamba huweza kubakia sikioni na ikikaa
 kwa muda mrefu itakuwa inazuia uchafu wa
 sikio kutoka,pia kuharibu ngoma ya sikio,
 huu
 utando unaotoka sikioni kazi yake kulinda
 sikio lisishambuliwe na vijidudu(bacter ia) na
 uchafu mwingine unaoingia sikioni kama
 vumbi, pamba ikiziba huchafu hautoki
 kuweza kuoza na kutoa maji maji(usaha) na
 sikio kuwasha.
 4. Kuharibu kuta za ndani zaidi ya sikio.
 Ni mara ngapi umeingiza pamba mpaka
 mwisho ndani kabisa ya sikio, na hapo
 ikigusa ndani zaidi mwisho tundu la sikio
 karibia na ngoma ya sikio utasikia maumivu,
 hii ni kwasababu ya pamba kuumiza kuta za
 ndani ya sikio mpaka kwenye ngoma ya sikio
 inaweza kuchanika hii ni hatari zaidi.
 5. Kukwaruza kuta za siko.
 Baada tu ya kutumia pamba kusafisha sikio
 utasikia muwasho ndani ya sikio hii
 inamaanisha umekwaruza kuta za sikio na
 pamba zinazotumika ni kavu, apo mtu
 huendelea kusafisha ili mradi asisikie
 muwasho matokeo yake ni kukwaruza zaidi
 kuta za sikio hii naweza kusababisha
 vidonda
 ndani ya sikio.
 N.B- Ushauri, ni vizuri ukangoja ushafu au
 utando wa sikio ukatoka wenyewe nje apo
 ukautoa kirahisi zaidi kuliko kulichokonoa
 sikio, ukishindwa hii njia tumia kipande cha
 nguo safi kiloweshe maji na taratibu usafishe
 sikio lako, kwa watoto usimwingize pamba
 masikioni kama umeshindwa kumtoa utando
 wa sikioni kwa njia niliyoshauri apo juu ni
 bora humpeleke hospitali kuna njia salama
 zaidi (bulb syringe) hii hufanya kwenye
  mahospitali chini ya uangalizi maalumu wa daktari!!
 
No comments:
Post a Comment