Pages

Tuesday, October 1, 2013

MADHARA MA 5 YA KUTUMIA PAMBA KUSAFISHIA MASIKIO/ EAR STICK

 
 
1. Kwanza husukuma ndani zaidi uchafu
 sikioni(ear wax),ule utando unaotoka ndani
ya sikio.
Unapochokonoa sikio kwa pamba huupeleka
uchafu kuingia ndani zaidi ya sikio, hii
husababisha vijidudu kushambulia kuta za
ndani ya sikio na ngoma ya sikio, hupelekea
mtu kutosikia vizuri.

2. Pia kutumia pamba kusafishia sikio
huatarisha kutokwa damu masikioni.
Unaposukuma ndani zaidi pamba kwenye
kuta za sikio ni ngozi laini, unaweza kuona
viti damu kwenye pamba, hii hutokana na
pamba kukwangua kuta za sikio lako.

3. Kutoka maji maji yanayowasha au usaha
sikio.
Hizi pamba huweza kubakia sikioni na ikikaa
kwa muda mrefu itakuwa inazuia uchafu wa
sikio kutoka,pia kuharibu ngoma ya sikio,
huu
utando unaotoka sikioni kazi yake kulinda
sikio lisishambuliwe na vijidudu(bacter ia) na
uchafu mwingine unaoingia sikioni kama
vumbi, pamba ikiziba huchafu hautoki
kuweza kuoza na kutoa maji maji(usaha) na
sikio kuwasha.

4. Kuharibu kuta za ndani zaidi ya sikio.
Ni mara ngapi umeingiza pamba mpaka
mwisho ndani kabisa ya sikio, na hapo
ikigusa ndani zaidi mwisho tundu la sikio
karibia na ngoma ya sikio utasikia maumivu,
hii ni kwasababu ya pamba kuumiza kuta za
ndani ya sikio mpaka kwenye ngoma ya sikio
inaweza kuchanika hii ni hatari zaidi.

5. Kukwaruza kuta za siko.
Baada tu ya kutumia pamba kusafisha sikio
utasikia muwasho ndani ya sikio hii
inamaanisha umekwaruza kuta za sikio na
pamba zinazotumika ni kavu, apo mtu
huendelea kusafisha ili mradi asisikie
muwasho matokeo yake ni kukwaruza zaidi
kuta za sikio hii naweza kusababisha
vidonda
ndani ya sikio.

N.B- Ushauri, ni vizuri ukangoja ushafu au
utando wa sikio ukatoka wenyewe nje apo
ukautoa kirahisi zaidi kuliko kulichokonoa
sikio, ukishindwa hii njia tumia kipande cha
nguo safi kiloweshe maji na taratibu usafishe
sikio lako, kwa watoto usimwingize pamba
masikioni kama umeshindwa kumtoa utando
wa sikioni kwa njia niliyoshauri apo juu ni
bora humpeleke hospitali kuna njia salama
zaidi (bulb syringe) hii hufanya kwenye
mahospitali chini ya uangalizi maalumu wa daktari!!

No comments:

Post a Comment