Pages

Tuesday, October 1, 2013

Pima maendeleo yako kwa kujiuliza maswali haya....



Kwa mtu makini na hodari anayependa kujiendeleza iwe kiimani, kimahusiano, kiafya, kikazi au kitaaluma hujiwekea malengo na kumbukumbu ya mafanikio yake  kila wakati anapopiga hatua.
Yafuatayo ni maswali kadhaa yatakayokusaidia kutafakari na kupima mafanikio au udhaifu wako ikiwa unadhumuni la kuwa mtu bora zaidi.
Jiulize maswali yafuatayo...

1. Umefanikisha nini katika miezi mitatu (3) iliyopita, na kwanini kitu hicho kilikuwa na maana kubwa kwako?
 2. Je ulipata changamoto gani katika kufanikisha malengo yako ya nyuma? Mambo gani yalikukwaza? Utafanya nini kusonga mbele?


3. Ni maeneo gani katika maisha yako yanayohitaji mkazo au umakini zaidi?
Mfano: Je unahitaji kukazia katika  uchumi wako, afya yako, kazi yako, familia yako au uhusiano wako na ndugu, jamaa au rafiki zako.. Utafanyaje ili kuweka mambo sawa?

4. Je ni zipi ndoto zako au matumaini yako? Je umeweka mikakati mizuri ya kupata utakacho?
5. Je ni maeneo gani ya kazi au shughuli zako unataka kubadilisha au kuboresha zaidi ili kuongeza tija na mafanikio yako ya baadae?

6. Je ni mafanikio ya kiasi gani unayofurahi kuyapata na kutoa msaada kwa wengine?
Itakuwa ni vyema kila baada ya miezi mitatu (3) upime maendeleo ya maisha yako. Weka jitihada na mafanikio yako katika darubini kulingana na mategemeo yako. Kisha endelea kuongeza bidii na kuwa na imani utafanikiwa, Unaweza pia ukawa na kitabu rasmi kwaajili ya kuweka kumbukumbu za maendeleo yako. Kila hatua ndogo unayopiga rekodi kwenye kitabu, hii itakusaidia kuona ni jinsi gani upo karibu au mbali na malengo yako. Kumbuka usisahau kujipongeza kwa kila mafanikio madogo au makubwa unayoyapata.

No comments:

Post a Comment