Pages

Tuesday, October 1, 2013

Haya ndio Maswali muhimu ya kujiuliza kila siku.


Kujiuliza maswali ni moja ya namna ya kutaka kupata majibu. Ni busara kama kila siku angalau kwa dakika chache utajiuliza maswali ya kukujenga kifikra na kupanua wigo wa manufaa katika maisha yako. Majibu ya maswali haya yenye tija yatakupa nuru na kukubadilisha kuwa mtu bora zaidi.
''Watch this video explaining the most important questions you can ask yourself throughout your day.''
 
1. Ni kitu gani kizuri ulichofurahia siku ya leo?
-Moja ya sifa ya maisha mazuri ni kufurahia kile unachofanya kila siku. Itakuwa ni faraja kubwa sana kutambua chochote kizuri kilichotokea kwako au kwa namna moja au nyingine kimekufurahisha kwa siku ya leo. Utakapo jua uzuri wa kitu ndio mwanzo wa kujua ni kwa kiasi gani maisha ni ya kipekee kwako.
 2. Umefanya kitu gani bora siku ya leo?
-Ni vyema ujue umejifunza nini leo? Ni makosa gani uliyofanya kwa siku ya jana na leo umeyarudia? Je una mpango gani wa kujirekebisha au kuepuka kurudia makosa yanayokusogeza mbali na ndoto zako? Kila siku jaribu kuboresha maisha yako ya sasa na ya baadae iwe kiafya ,kiuchumi au kitabia.
 
3.Ni jambo gani muhimu kwako unalotaka kukamilisha siku ya kesho?
-Kabla hujaanza siku nyingine hakikisha umeshajua siku inayofuata utafanya nini. Chukua karatasi na kalamu orodhesha mambo yote utakayofanya siku ya kesho kisha weka ratiba yako sehemu ambayo unaweza ukaiona kirahisi kila utakapo ihitaji. Kumbuka kuzingatia na kutekeleza kila jambo lililomuhimu kwako.
 4.Unategemea kufanya kitu gani kipya au tofauti  siku ya kesho?
-Maisha ni safari ndefu yenye miujiza ya mafanikio inayotokea kila siku kwa watu wanaofanya bidii kwa kile wanachotafuta. Milango ya bahati hufunguka kwa wale wanaojaribu mambo tofauti katika maisha yao. Mabadiliko yanaweza kuwa ya kibiashara, kijamii au kisiasa anza leo kwa kile unachoona unataka kiwe sawa. Mfano: Siku ya kesho unataka kubadilisha mlo wako mchana kwa kula chakula tofauti na siku nyingine. Au kesho unataka kubadilisha aina ya mazoezi ya mwili badala ya kunyoosha viungo vyako vya mwili unaamua kukimbia mchakachaka. Hivi ndivyo tunavyotakiwa tubadilike.
   
5.Ni watu gani muhimu sana kwako? Umepanga kuwafanyia nini ili kuimarisha mahusiano baina yako na wao?
-Thamini watu wote lakini wapende zaidi waliokaribu na wewe katika maisha yako kama vile wazazi, watoto au mpenzi wako. Je umeonyesha kuwa unawajali na kuwapenda? Wakati mwingine huwa tunatingwa na mambo mengi na kusahau watu waliomuhimu kwetu. Kila unapojiuliza swali hili litakufanya uwakumbuke wote waliomujimu kwako. Jijengee mazoea na mahusiano mazuri na washirika wako kwa kushirikiana nao vizuri nao watakupenda.
Maswali haya ni ya msingi sana, kila unapojiuliza na kupata majibu ya maswali haya nina imani yataleta athari ya kimaendeleo katika maisha yako. Jiulize leo hakika mafanikio yatakuwa karibu yako.
 


No comments:

Post a Comment